Thursday 10 August 2017

Location: Dar Es Salaam

Description
Mwananchi 28/7/2017
Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke anawatangazia Wananchi/ Watanzania wote wenye sifa zinazotakiwa kuomba kujaza nafasi mbalimbali za kazi kama zilivyoainishwa hapo chini:-
Msaidizi Wa Kumbukumbu Daraja II (Nafasi 3)
SIFA ELIMU/UJUZI
• Elimu ya kidato cha Nnne (IV), au Kidato cha Sita (VI,)
• Cheti cha utunzaji kumbukumbu katika mojawapo ya fani ya afya, Masjala, Mahakama, na Ardhi.
KAZI NA MAJUKUMU
• Kutafuta kumbukumbu/nyaraka/mafaili yanayohitajiwa na wasomaji.
• Kuthibiti upokeaji, uandikishaji wa kumbukumbu /nyaraka.
• Kuchambua, kuorodhesha na kupanga kumbukumbu/ nyaraka katika makundi kulingana na somo
• husika (classification and boxing) kwa ajili ya matumizi ya Ofisi.
• Kuweka/kupanga kurnbukurnbu/nyaraka katika reki (file racks/cabnet) katika masjala/ nyumba za kuhifadhia kumbukumbu.
• Kuweka kumbukumbu(barua,nyaraka nk)kataka mafaili.
• Kushunghulikia maombi ya kumbukumbu/nyaraka kutoka taasisi za serikali.
NGAZI VA MSHAHARA
Ataanza mshahara TGS B (1) kwa mujibu wa viwango vya Serikalini.
UMRI
Waombaji wote wanatakiwa wawe na umri usiopungua miaka 18 na usiozidi miaka 45.
MAELEZO YA JUMLA
Maombi yote yawasilishwe yakiwa yameambatanishiwa na CV pamoja na nakala za vyeti vya kuhitimu elimu na mafunzo (vyeti vinavyoonyesha kiwango cha kufaulu na sio ‘leaving certificate’)
MUHIMU
Muombaji anatakiwa atume vyeti vyake halisi na halali kwani uhakiki utafanyika katika vyuo alivyopitia parnoja na Baraza la Mitihani. Udanganyifu wowote ukibainika hatua za kisheria zitachukuliwa.
MAOMBI VATUMWE KWA ANWANI IFUATAVO:-
MKURUGENZI WA MANISPAA
HALMASHAURI VA MANISPAA VA TEMEKE
S.L.P 46343, DAR ES SALAAM


Application deadline 2017-08-28

Find us on Facebook

Blog Archive

Popular Posts