Friday 11 August 2017

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI.

Serikali inatarajia kuajiri Walimu 92 wa Shahada na 174 wa Stashahada wa masomo ya Fizikia, Hisabati, Kilimo na Biashara kwa Shule za Sekondari na Walimu 2,767 wa Cheti kwa Shule za Msingi.
Waombaji kwa shule za Sekondari wawe waliohitimu mafunzo ya Ualimu mwaka 2016 au kabla, na wale wa Shule za Msingi wawe waliohitimu mafunzo yao mwaka 2014 au kabla.
Sifa za Waombaji:
Walimu wa Sekondari:
Shahada ya Elimu (Bachelor with Education) au Shahada ya Ualimu (Bachelor of Education) yenye somo moja la kufundishia au zaidi au Shahada isiyo ya Ualimu/Elimu yenye somo moja la kufundishia au zaidi pamoja na Stashahada ya Uzamili ya Elimu (Postgraduate Diploma in Education) kutoka Vyuo vya Elimu ya Juu vinavyotambulika na Serikali. Masomo ya kufundishia ni kati ya Fizikia, Hisabati, Kilimo au Biashara.
Stashahada ya Ualimu katika masomo yaliyoainishwa kwenye kipengele Na. 2.1 (i) hapo juu.
Cheti cha Kidato cha Sita
Cheti cha Kidato cha Nne
Walimu wa Shule za Msingi:
Astashahada ya Ualimu iliyotolewa na Chuo kinachotambuliwa na Serikali.
Cheti cha Kidato cha Nne (wenye cheti Kidato cha Sita watapewa kipaumbele).
Utaratibu wa Kutuma Maombi:

Maombi yatumwe kupitia Posta kwa njia ya Rejesta (EMS).  Juu ya bahasha iandikwe kwa mkono "Maombi ya Kazi ya Ualimu - Sekondari au Maombi ya Kazi ya Ualimu - Msingi".
Mwombaji aambatishe nakala za Vyeti vilivyothibitishwa (Certified) na Mwanasheria pamoja na "Transcript".
NB:  Barua za maombi zisiwasilishwe kwa mkono.  Barua zitakazowasilishwa kwa mkono hazitapokelewa.

Masuala Mengine ya Kuzingatia:
Mwombaji aandike majina yake yote matatu.  Kama Vyeti vina majina mawili, utaratibu wa kisheria wa kuongeza jina uzingatiwe.
Mwombaji aambatishe nakala ya Cheti cha Kuzaliwa.
Mwisho wa kupokelewa maombi ni tarehe 31/08/2017.

Maombi yatumwe kwa:

Katibu Mkuu,

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia,

S. L. P. 10,

40479 DODOMA.
Job Title:  CLINIC NURSE/COUNSELOR (17)

Employer: MDH
Reports to: Nurse Supervisor
Qualification and Work Experience:
Nurse Counselor should have at least a diploma in Nursing and must have a valid practice license; he/she should have an experience of 3 years in the field of expertise.
Expectations:
A HIV/AIDS nurse counselor requires extensive, current knowledge of the symptoms and treatments of AIDS and HIV infections, the methods by which the virus is (and is not) transmitted and prevention measures. HIV/AIDS counselors
must enjoy working with other people, have a compassionate nature and be good listeners. A broad knowledge of diverse cultural beliefs and attitudes is often necessary when working with diverse populations.
Duties and Responsibilities
1. Adhering to nursing ethics as punctuality and cleanliness etc.
2. Ensuring that patients receive appropriate clinical care during a clinic visit, including scheduled or unscheduled physician examination and laboratory test.
3. Educating patients in all aspects of HIV disease and treatment management, as well as basic healthy lifestyles.
4. Counseling patients with regard to HIV diagnosis, management of medications, medication and clinic visit adherence, psychosocial issues, and basic health self-care.

5. Counseling and educating family members and care givers to promote secondary prevention of HIV infection, to improve the care of patients with HIV, and to strengthen social support networks of patients.
6. Accurate and complete documentation of patient information and patient encounters in the patient medical record.
7. Assisting patients to connect with other resources through the referral network.
8. Assisting the physician in the provision of clinical care for patients.
9. Doing any other duty as assigned by the nurse supervisor, site manager and OPD nurse officer in-charge.

HOW TO APPLY:
Interested candidates should submit their application letters, CVs, Certified photocopies of certificates and names and contact information (email addresses and telephone numbers) of two references.
e-mail hr@mdh-tz.org
Applications should be submitted by 14th August, 2017 to the HR Manager, MDH through e-mail hr@mdh-tz.org or drop by hand at our MDH Mikocheni Office near New Regency Park Hotel. Please note; only shortlisted candidates will be contacted.

Find us on Facebook

Popular Posts